Thursday, June 15, 2006

UPUNGUFU WA MAJI ULIMWENGUNI NI CHANZO CHA VITA YA BAADAE.
Uhalibifu wa mazingira na vyanzo vya maji pamoja na harakati za kibinadamu ktk kujitafutia maendeleo kutokana na majaribia mbali mbali yanayo haribu mazingira ni vyanzo vikuu vikubwa vinavyo sababisha upungufu wa maji ulimwenguni.

Kama ilivyo kwa thamani ya bidhaa za madini mbali mbali, Petrol, Diesel pamoja mafuta ya taa ambayo inayo fanya au kuleta vita hapa duniani ndivyo itakavyo kuwa ktk hii bidhaa muhimu (maji) ktk maisha ya binadamu ambayo ina muwezesha kuweza kuishi na hapo ndipo binadamu tutaweza kupigana vita kwa sababu ya upungufu wa maji.


Kama binadamu wa sasa hawezi kutunza mazingira yake pamoja na vyanzo vya maji basi matatizo makubwa yanaweza kutukumba, Baadhi ya hayo matatizo tunayaona sasa ambapo kila kona ya ulimwengu kuna upungufu wa maji. i.e Kama tunavyo fahamu uchumi wa nchi nyingi ulimwenguni unategemea kilimo ambapo hiko kilimo kinategemea maji sasa kama hakuna maji basi uchumi wa mataifa mengi utakuwa mbaya ambapo utazoretesha uduma mbali mbali za kijamii, n.k

Nawaomba muangalie hii habari kuhusu matatizo ambayo tunayo na yatakayo tukumba.

Mwisho, tuweze kutunza mazingira yetu na kuweza kuelimisha jamii nzima kuhusu mazingira na tuweze kutumia maji tuliyo nayo kwa uangalifu.

Thursday, May 18, 2006


HISTORIA YA AIRBUS A380 NDANI YA UK
Ndege ya abiria aina ya Airbus A380 yenye viti vya abiria 555 ambayo ni kubwa kuliko zote ulimwenguni imeweza kuingia ktk historia ya kuwa ni ndege ya kwanza ya aina hiyo kutua ktk ardhi ya Uingereza ktk uwanja wa ndege wa Heathrow hii leo 18/05/2006 saa 13:20 mida ya Uingereza ikitokea Berlin, Germany.

Maandalizi ya kuwezesha ndege hiyo kutua ktk uwanja wa Heathrow imewagarimu waingereza ( British Airports Authority) jumla ya 450 Million pounds na pia imetua ktk sehemu impya ( Inayo julikana kama pier 6 ktkTerminal 3) iliyo jengwa na kugarimu jumla ya 105 Million pounds.

Airbus A380 itakuwa ni mshindani mkubwa wa ndege za Boeing, na kuonesha Boeing wapo ktk ushindani nao wametengeneza ndege aina ya 787 Dreamliner kuweza kushindana ambayo inategemewa kuingia ktk soko ifikapo mwaka 2008 na kuweza kubeba abiria kati ya 200 mpaka 350.

Jumla ya gharama zilizo wezesha kutengeneza ndege ya Airbus A380 ni 6 Billion pounds ambapo mpaka sasa kampuni ya Airbus S.A.S imepokea order karibia 159 kutoka kwa mashirika 16 ya ndege zinazotaka kununua aina hii ya ndege.

Bonyeza hapa kusoma orodha ya makampuni na idadi ya ndege walizo order.

Bonyeza hapa kuona video mbali mbali za Airbus A380 pia kama ukitaka kuangalia video nyinginezo zinapatikana kwa kubonyeza hapa.

Mwisho, ingawa hii ni kama historia lakini imeleta mitazamo tofauti ambapo kuna makundi mawili, yanayo kubaliana na technology hii na wanao ipinga kutokana na sababu za mazingira.

Tuesday, May 16, 2006

Kama ukitaka blog yako ipendeze zaidi, basi unaweza kuweka hizi code ili kuweza kufanya scrollbar yako kubadilika rangi au iwe na rangi tofauti tofauti. Unaweza kuangalia scrollbar ktk blog yangu na kuona ninacho sema.

Unaweza kubadili rangi tofauti tofauti kutokana na mapendekezo yako, na utaweza kufanya hivyo ktk sehemu zenye maandishi kama #FFFFFF; #6DA4FF; #ACA899; black; #FFFFFF; na kufuta #FFFFFF, #6DA4FF, #ACA899, black au #FFFFFF na kuandika rangi unayotaka eidha kwa kutumia code kama nilivyo andika mwanzo au kwa maandishi mfano pink, green, red, n.k.

Kumbuka ukiandika kwa code au kwa maandishi andika kwa usahii na kwa kiingereza tu na msifute alama hii ; yaani ukiandika red iwe red; au #ff0000; hivyo ndivyo ingekuwa kwa kutumia code nikiwa nina maanisha rangi nyekundu.

Yafuatayo ndio maelekezo ya kufanya:

1: Sign In ktk Blog yako

2: Ukifika ktk Dashboard,Click->Change Settings->Template

3: Ukifika ktk template, tafuta wapi yalipo haya maandishi head yakianza na tag < na kuishia na tag > na baada ya kuyapata hayo maandishi chini yake weka code zifuatazo.

4: Mwisho, click save template changes alafu click republish your blog.

Na hapo utakuwa umemamaliza kila kitu.

Tuesday, May 09, 2006

NA NYINGINE HIYO!!
Leo nawaletea code nyingine kwa wale wenye blog ndefu au blog za picha ambazo ni ndefu.

Code hizi ni kuwawezesha wasomaji wenu kuweza kupelekwa juu (Mwanzo) pale wafikapo mwisho bila ya kuangaika kwenda juu. Mfano wake upo ukiangalia chini ya hii blog (Vijimamboz) utaona kuna kijisehemu kina kwambia rudi juu na uki-click hapo unakwenda juu.

Maelekezo ni kama kawaida, Ambayo ni:
1(a): Sign In ktk Blog yako

1(b): Ktk Dashboard,Click->Change Settings->Template

1(c): Ukifika ktk template, Chagua ni wapi unataka hiyo button iweze kukaa (Ni vizuri ukiweka chini kabisa maana wasomaji wenu wakishafika mwisho wa blog tu waweze kukibonyeza na kupelekwa juu) na alafu muweke hizi code.

1 (d): Mwisho, click save template changes alafu click republish your blog.

Na hapo utakuwa umemamaliza kila kitu.